Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Jumatano April 19 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Apr 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatano April 19 2023

Mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane, 29, ndiye anayesakwa zaidi na Paris St-Germain msimu huu wa joto. (Le Parisien)

Meneja David Moyes kuna uwezekano mkubwa wa kuondoka West Ham msimu huu wa joto huku mchakato wa kubaini watakaomrithi ukiendelea. (Mail)

Jose Mourinho anaweza kuwa meneja mpya wa Paris St-Germain msimu ujao huku bosi huyo wa Roma akiwa kileleni mwa orodha ya mkurugenzi wa michezo wa PSG, Luis Campos. (RMC Sport)

Crystal Palace wanataka Roy Hodgson abaki katika klabu hiyo baada ya majira ya kiangazi ili kumshauri yeyote atakayechukua nafasi yake kama meneja ajaye wa Palace. (Telegraph)

Steven Gerrard anaripotiwa kuwa kwenye orodha ya wanaotajwa kusaka nafasi ya kocha mkuu ajaye wa klabu ya Olympiakos ya Ugiriki miezi sita baada ya kutimuliwa na Aston Villa. (Express)

Mazungumzo kati ya Alexis Mac Allister, 25 wa Brighton na Arsenal baso hayajafika popote. (Cesar Luis Merlo - via Twitter)

Barcelona inazidi kuamini kuwa mshambuliaji wa Argentina na Paris St-Germain Lionel Messi, 35, atajiunga tena na klabu hiyo msimu wa joto. (Sport)

United wanakaribia kukubaliana kandarasi mpya na mlinda mlango wa Uhispania David de Gea, 32, ambaye mkataba wake wa sasa unamalizika mwishoni mwa msimu huu. (ESPN)

Southampton wamemwambia kiungo James Ward-Prowse, 28, kwamba anaweza kuondoka msimu wa joto ikiwa klabu hiyo itashuka daraja. Tottenham, West Ham na Newcastle wote wanamtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa England. (Sport)

Leeds itamsajili winga wa kimataifa wa Uhispania aliyechini ya miaka 19 Ilias Akhomach, 19, baada ya kushindwa kukubaliana na Barcelona kuhusu kuongezwa mkataba. (Sport)

Maskauti wawili wa Manchester United walimtazama winga wa akademi ya Birmingham City na timu ya taifa ya England ya Under-16 Trevan Sanusi, 15, siku ya Jumatatu. (Football Insider)

Beki wa kati wa Ivory Coast Eric Bailly, 29, atarejea United msimu huu wa joto huku Marseille wakikach kufanya mkataba wake wa mkopo kuwa wa kudumu. (Fabrizio Romano)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
41m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’