Real Madrid, AC Milan zatinga nusu fainali UEFA

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th April 2023


Real Madrid, AC Milan zatinga nusu fainali UEFA

Chelsea imeondoshwa kwenye Ligi ya Mabingwa kwa kupoteza kwa jumla ya mabao 4-0 kutoka kwa mabingwa watetezi Real Madrid

Mabao mawili ya Rodrygo yalitosha kuwaadhibu The Blues kwa kichapo cha 2-0 Stamford Bridge huku yakiwashuhudia Real Madrid wakitinga nusu fainali katika michuano ambayo imekuwa kawaida yao kushinda wanapofika hatua hiyo

Kikosi cha Frank Lampard kilihitaji kupindua kipigo cha mabao mawili kutoka kwa mechi ya kwanza ili kuwa na matumaini lakini haikuwezekana 

Ilikuwa mechi ya nne mfululizo Lampard anapoteza tangu akabidhiwe mikoba ya kuwa kocha wa muda

AC Milan nao wakawaduwaza mabingwa watarajiwa wa Serie A Napoli kwa kuwalazimisha sare ya bao 1-1 katika uwanja wao wa nyumbani

Milan wametinga nusu fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-1 kufuatia ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa San Siro

Mechi nyingine mbili za robo fainali zitapigwa leo, Bayern Munich wakiwa nyumbani watakuwa na kazi ya kupindua matokeo ya kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Manchester City wakati Inter Milan watahitaji kulinda ushindi wa mabao 2-0 waliopata ugenini dhidi ya Benfica


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.