JK akutana na wanariadha walioshinda Marekani

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th April 2023


JK akutana na wanariadha walioshinda Marekani

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete amekutana na Wanariadha Gabriel Geay na Wence Tarimo walioshiriki katika Mashindano ya Riadha yaliyofanyika Boston, Marekani Aprili 17, 2023

Gabriel Geay aliibuka mshindi wa pili katika mashindano hayo

Mheshimiwa Rais Mstaafu amempongeza Gabriel Geay kwa ushindi mkubwa na kwa kupeperusha vyema bendera ya Tanzania

Pamoja na wanariadha hao, walikuwepo pia wahamasishaji mbalimbali akiwemo 'Bongo Zozo'

Aidha, amewapongeza pia kwa kuhamasisha ushindi huu na kufanikisha kuinua bendera ya Tanzania juu

Rais Kikwete yuko Boston, Marekani ambapo anashiriki katika kutoa mafunzo kwa Mawaziri wa Fedha kutoka nchi mbalimbali zinazoendelea kupitia Mpango wa Uongozi wa Harvard 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.