Msafara wa kikosi cha mabingwa watetezi ligi ya mabingwa Wydad Athletic kinatarajiwa kuwasili nchini leo kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali michuano hiyo dhidi ya Simba
Simba itakuwa mwenyeji wa mchezo huo ambao utapigwa Jumamosi, April 22 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni
Wydad iliondoka Morocco na msafara wa watu 50 wakitumia ndege binafsi
Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc watakuwa na shughuli pevu ya kusaka ushindi dhidi ya wababe hawa wa soka barani Afrika ngazi ya klabu kwa sasa
