Walima alizeti wa Singida Big Stars wanakabiliwa na mechi mbili dhidi ya Yanga kwenye ligi kuu na kombe la Shirikisho la Azam (ASFC)
Mchezo wa Ligi kuu utapigwa May 04 na mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) ukipigwa May 07 . Mechi zote zitapigwa katika uwanja wa LITI
Msemaji wa Singida BS, Hussein Massanza amesema wamepokea barua asubuhi ya leo Jumatano ikiwaelekeza kuhusu michezo hiyo
Amesema wameanza maandalizi kujiandaa na michezo hiyo na imani yao watafanya vizuri
Singida BS wanahitaji kushinda mchezo dhidi ya Yanga ili kujihakikishia nafasi ya kumaliza tatu za juu kwenye ligi huku pia wakiwa na nafasi ya kushiriki michuano ya CAF kama watatwaa kombe la Shirikisho la Azam (ASFC)