JKT - Local

JKT Tanzania yarudi Ligi Kuu kibabe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Apr 2023
JKT Tanzania yarudi Ligi Kuu kibabe

Uongozi wa JKT Tanzania FC umeweka wazi kwa sasa tayari malengo yao ya kutwaa ubingwa wa Ligi ya Championship msimu huu na kupanda daraja kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao yametimia kwa asilimia 90

JKT Tanzania inayonolewa na Kocha Malale Hamsini, ndio vinara wa Ligi ya Championship wakiwa na pointi 62 huku nafasi ya pili ikishikwa na Pamba ya Mwanza yenye pointi 51, kila timu imebakiza mechi tatu ili kumalizika kwa msimu huu.

Katibu wa JKT Tanzania, Kapteni Speratus Lubinga, amesema timu yao imejipanga kufanya vyema kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika michezo mitatu iliyobaki na kupanda Ligi Kuu Tanzania Bara kwa heshima.

Lubinga alisema anafahamu kufanya vyema kwa timu yao kulitokana na uongozi wa kikosi cha JKT kuwa bega kwa bega na benchi la ufundi la timu hiyo na kuwahamasisha wachezaji wakati wote wanapokuwa ndani na nje ya uwanja.

"Sina mengi lakini natoa shukrani za dhati kwa uongozi mzima wa Jeshi la Kujenga Taifa likiwa chini ya Mkuu wa JKT Meja Jenerali, Rajabu Mabele, pamoja na Mkuu wa Tawi la Utawala, Brigedia Jenerali Hassan Mabena, ambao wamekuwa wakiongeza hamasa kwa wachezaji ya kupata matokeo mazuri," alisema kiongozi huyo.

Aliongeza mpaka sasa wametimiza asilimia 90 ya malengo yao kuelekea kukata tiketi ya kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu ujao.

Alitaja mechi tatu walizobakisha ni dhidi ya Kitayosce ya Tabora, Pamba, ambazo watacheza ugenini na watamaliza msimu nyumbani kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo kwa kuwakaribisha Mashujaa.

"Kikosi kipo imara, lengo letu ni kuhakikisha tunaibuka na ushindi na kutwaa ubingwa wa Ligi ya Championship kwa msimu huu, tutakuwa tumetimiza maagizo ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa ambaye alitaka kuona kikosi kinarejea Ligi Kuu katika msimu ujao, sina shaka na wachezaji wangu, wanajituma kwa kuhakikisha timu inarudi," aliongeza.

Ametoa wito kwa wadau na mashabiki wa JKT kujitokeza kwa wingi ili kuongeza hamasa kwa wachezaji katika mechi zilizobakia

IPP Media

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
27m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’