Simba - Local

Simba yapania kurudia rekodi ya 2003

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Apr 2023
Simba yapania kurudia rekodi ya 2003

Wakati Wydad Casablanca kutoka Morocco ikiwa imewasili tayari kwa mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika, Simba iko tayari na kamili kurudia ilichokifanya mwaka 2003 kwa kuwavua taji waliokuwa mabingwa wa Afrika, Zamalek ya Misri

Simba itawakaribisha mabingwa watetezi, Wydad katika mechi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Jumamosi April 22

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema baada ya miaka 20, imefika wakati Simba ikaweka rekodi nyingine ya kuwavua ubingwa Wydad kama walivyofanya mwaka 2003.

"Tuna shughuli moja tu ya kwenda kumnyoa Wydad Casablaca ili tuandike historia nyingine ya kumvua mtu ubingwa. Tunajua mechi ni ngumu, tunacheza na mtu aliyetudizi viwango vya CAF, tunacheza na mabingwa watetezi, lakini Wanasimba tukiunganisha nguvu na kushikamana, Wydad Casablaca hawana pa kutokea," alisema Ahmed

Wydad Casablanca ilitua jana mchana ikiwa na msafara wa watu zaidi ya 50, ambao ni wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na baadhi ya mashabiki.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
39m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’