Jana Manchester City ilisonga hatua moja karibu na uwezekano wa kutwaa mataji matatu msimu huu baada ya kutinga fainali ya Kombe la FA
Hat-trick kutoka kwa Riyad Mahrez ilitosha kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya Sheffield United kwenye Uwanja wa Wembley na kutinga fainali
Pep Guardiola alipanga kikosi chenye nguvu kwa pambano hilo, akiwemo Jack Grealish na Erling Haaland ambaye alikuwa akicheza mechi yake ya kwanza Wembley
Man City watamenyana na Manchester United au Brighton kwenye mchezo wa fainali
Kusonga mbele katika Kombe la FA kunamaanisha kwamba City wako kwenye njia thabiti ya kupata mataji matatu ya kihistoria, baada ya kupata nafasi ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa ambapo watamenyana na Real Madrid kwa mikondo miwili
Pia wanaonekana kuwa na nguvu kwenye Ligi Kuu sare ya 3-3 kati ya Arsenal na Southampton Ijumaa usiku ina maana kwamba The Gunners sasa wako pointi tano mbele ya City kwenye Premier League, hata hivyo wakiwa na michezo miwili mkononi vijana wa Guardiola wanashikilia karata katika mbio za mwisho



