Tottenham wanafikiria kumtimua Cristian Stellini baada ya kuchapwa mabao 6-1 na Newcastle
Spurs walifungwa mabao matano katika dakika 21 za mwanzo baada ya Stellini kuanza mabeki wanne kwa mara ya kwanza msimu huu
Muitaliano huyo alirejea katika mfumo wa walinzi watatu baada ya muda mfupi lakini uharibifu ulikuwa umefanyika
Uongozi wa Tottenham unafikiria kukata uhusiano mapema kulingana na ripoti ya Evening Standard
Stellin mwenye umri wa miaka 48 aliteuliwa kuwa kaimu kocha mkuu hadi mwisho wa msimu baada ya Antonio Conte kutimuliwa mwezi uliopita lakini uamuzi huo unaweza kutenguliwa hivi karibuni
Ryan Mason ametajwa kuwa chaguo la kumrithi Stellini hadi mwisho wa msimu.