Transfer - Local

Dilunga kurejeshwa kikosini Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Apr 2023
Dilunga kurejeshwa kikosini Simba

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amependekeza kurejeshwa kikosini kwa kiungo mshambuliaji Hassan Dilunga pale dirisha la usajili litakapofunguliwa

Mwaka mzima Dilunga alikuwa nje baada ya kuumia mazoezini, sasa ni miezi kadha imepita mchezaji huyo anafanya mazoezi na timu hiyo, jambo lililomshawishi Robertinho kukubali kiwango chake

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zimebainisha kuwa Robertinho amewaambia viongozi kwamba ukianza usajili waanze na Dilunga anaona anamfaa kwenye kikosi chake

"Kwenye mazoezi Dilunga anaonyesha kiwango cha juu, kinachomfanya kocha aamini ni kati ya wazawa ambao wanaweza wakawa msaada mkubwa ndani ya kikosi chake msimu ujao"

"Dilunga aliumia akiwa na Simba, ndio maana alipewa nafasi ya kufanya mazoezi na wenzake, pamoja na hilo mchezaji mwenyewe hakujibweteka anapenda mazoezi na alionyesha ana kitu kikubwa kinachomfanya kocha apende kumuona kwenye kikosi chake na nafakiri ameshawaambia uongozi kuwa anamhitaji kwa ajili ya msimu ujao, kama watawezana basi ataonekana kwenye jezi ya Simba," alibainisha mtoa taarifa

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
39m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’