Simba - Local

Simba yatua Morocco na mkakati wa ushindi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 Apr 2023
Simba yatua Morocco na mkakati wa ushindi

Mkufunzi wa Simba Robertinho Oliviera amesema wamejiandaa kimbinu zaidi, kuelekea mchezo wa marudiano wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wydad Casablanca.

Simba tayari imewasili salama nchini Morocco tayari kwa ajili ya mchezo huo dhidi ya wenyeji wao hao itashuka dimbani Ijumaa ya Aprili 28 mwaka huu kwenye uwanja wa Mohammed V, nchini humo katika mji wa Casablanca.

Robertinho amesema kuwa maandalizi waliyoyafanya kuelekea mchezo huo wa marudiano ni mazuri na hawatakuwa wanyonge kwa sababu malengo yao ni kutaka ushindi.

Alisema ana imani kubwa na wachezaji wake kuonyesha kiwango kizuri zaidi walichokionyesha kwenye mechi ya kwanza waliyocheza uwanja wa Benjamin Mkapa na kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

"Tunajua mechi dhidi ya Wydad Casablanca itakuwa ngumu sana, lakini tumejiandaa na mipango yetu ni kufikia malengo tuliyojiwekea kama timu," alisema.

"Sisi sio timu nyepesi tena watu watuheshimu tunaweza kwenda ugenini na tukafanya kitu, tunawaheshimu Wydad, lakini hatutacheza kinyonge pale Casablanca tumekuja kupigania heshima ya klabu hii kubwa," aliongeza Robertinho

Alisema wanatambua umuhimu na ugumu wa mechi hiyo na wanacheza kwa pamoja na kuwa makini na safu ya ushambuliaji ya Wydad Casablanca, mechi iliyopita walitengeneza nafasi na kushindwa kuzitumia.

Robertinho alisema wamewaona Wydad Casablanca wanapocheza nyumbani na kutakiwa kuwachunga sana kila sehemu ndani ya uwanja ili kurejea nchini wakiwa tayari wametinga nusu fainali.

Alisema anachokiangalia zaidi ni kuhakikisha wanakuwa makini katika mchezo huo ambao wanahitaji kutafuta matokeo mazuri ili kuwapeleka kucheza nusu fainali ikiwa ni mipango yao kwa sasa

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
29m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
41m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’