Simba - Local

Robertinho anaamini ushindi upo Morocco

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Apr 2023
Robertinho anaamini ushindi upo Morocco

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ameeleza kufurahishwa na morali ya wachezaji wake kuelekea mechi ya marudiano robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Wydad Athletic

Kesho Ijumaa, majira ya saa 3 usiku, Simba itashuka uwanja wa Mohammed V huko Morocco kuwakabili Wydad katika mchezo ambao Simba itaingia ikiwa mbele kwa ushindi wa bao 1-0 uliopatikana kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza baada ya kikosi chake kukamilisha mazoezi yao ya kwanza tangu watue Morocco, Robertinho amesema kikosi chake kiko katika hali nzuri. Wachezaji wanajituma na kuonyesha utayari mkubwa wa kuwakabili Wydad

"Ninafurahishwa na vile wachezaji wanavyopokea maelekezo. Ari ni kubwa na kila mmoja anaonekana kuwa tayari kwa ajili ya mchezo siku ya Ijumaa. Tunafahamu tuna mechi ngumu hapa Morocco, tunaandaa mpango mzuri wa kimbinu kukabiliana na mchezo huo"

"Nimesema mara nyingi, tunahitaji kucheza kwa malengo tunapokuwa na mpira na hata pale tunapokuwa hatuna mpira. Tunao uwezo wa kupata matokeo mazuri hapa, wachezaji wetu wako tayari kuhakikisha tunafanikiwa," alisema Robertinho

Simba itakamilisha mazoezi ya mwisho leo katika uwanja wa Mohammed V tayari kwa mchezo huo ambao Simba itahitaji ushindi au matokeo yoyote ya sare ili kutinga nusu fainali

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’