Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu May 1 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st May 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu May 1 2023

Manchester City wanajiandaa kufanya mazungumzo na mshambuliaji wa Norway Erling Haaland, 22, kuhusu mkataba mpya. (Football Insider)

Mshambulizi wa Crystal Palace na Ivory Coast Wilfried Zaha anahusudiwa na vilabu vya Arsenal, Juventus, Chelsea na Barcelona huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 akitarajiwa kuondoka Selhurst Park mwishoni mwa msimu mkataba wake unapomalizika. (Telegraph)

Chelsea ina imani kuwa kiungo wake wa kati wa England Mason Mount, 24, atazikataa Bayern Munich na Liverpool na kusaini mkataba mpya kusalia katika klabu hiyo. (Football Insider)

Mshambuliaji wa Juventus Dusan Vlahovic, 23, anataka kuuzwa kwenda Arsenal na Bayern Munich huku muda wa Mserbia huyo katika klabu hiyo ya Italia unaonekana umefikia mwisho (Tutto Mercato Web)

Chelsea ni miongoni mwa klabu kadhaa za Ligi kuu England zinazomfuatilia kwa karibu mshambuliaji wa kati Stevenage, 16, Makise Evans. (Sun)

Newcastle United wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Roma mwenye umri wa miaka 29 kutoka Argentina Paulo Dybala. (Calcio Mercato)

Manchester United inataka kumsajili beki wa pembeni wa Paris St-Germain, Mmoroccofull Achraf Hakimi, 24. (Football Insider)

Sheffield United iko tayari kumuongezea mkataba mshambuliaji wa Scotland Oli McBurnie mwenye umri wa miaka 26 baada ya kufanikiwa kupanda daraja kucheza Ligi kuu England msimu ujao. (Sun)

Chelsea inahusishwa na mshambuliaji wa Bayern Munich na Senegal Sadio Mane, 31, ambaye alijiunga na timu hiyo ya Ujerumani akitokea Liverpool msimu uliopita wa joto. (Football London)

Klabu ya Saudi Pro League Al Nassr inamfuatilia beki wa kushoto wa Brazil Alex Telles, 30, ambaye yuko kwa mkopo Sevilla akitokea Manchester United na huenda akaungana tena na mchezaji mwenzake wa zamani wa Mashetani Wekundu Cristiano Ronaldo. (AS)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.