Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano May 03 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 May 2023
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano May 03 2023

Mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi, 35, ataondoka Paris St-Germain mwishoni mwa msimu huu baada ya mabingwa hao wa Ufaransa kuamua kutoongeza mkataba wake. (FootMercato)

Manchester United wameainisha nyota wa tatu mbadala wa mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane, 29 - Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa wa Eintracht Frankfurt Randal Kolo Muani, 24, mshambuliaji wa Roma na England Tammy Abraham, 25, na mchezaji wa kimataifa wa Argentina anayechezea Inter Milan Lautaro Martinez, 25. (FourFourTwo)

Mazungumzo ya Tottenham na meneja wa zamani wa Bayern Munich Julian Nagelsmann kuhusu kuwa meneja wao mpya yamekwama kwa sababu ya sintofahamu kuhusu nafasi ya mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo. (Telegraph)

Sam Allardyce yuko kwenye mazungumzo ya kuwa meneja ajaye wa Leeds United na amepewa bonasi ya pauni milioni 1 ikiwa ataibakisha klabu hiyo ya Elland Road kwenye Ligi kuu England. (Star)

Allardyce atapata bonasi ya zaidi ya £2.5m ikiwa ataweza kuibakisha ligi kuu Leeds United na anamtaka meneja wa zamani wa Oxford United Karl Robinson kuwa msaidizi wake pale Elland Road. (Times)

Wamiliki wenza wa Chelsea Todd Boehly na Behdad Eghbali walikutana Los Angeles mwishoni mwa wiki iliyopita kujadili uteuzi wa meneja wa zamani wa Tottenham Mauricio Pochettino ili awe meneja ajaye wa klabu hiyo ya Stamford Bridge. (Evening Standard)

Mmiliki wa Arsenal Stan Kroenke anatarajiwa kumpa meneja wa Gunners Mikel Arteta kitita cha pauni milioni 200 ili kuimarisha kikosi chake msimu wa joto. (Football transfers)

West Ham wameanza kutafuta kiungo mbadala wakijiandaa kumkosa mchezaji wa kimataifa wa England Declan Rice, 24 anayesakwa na Arsenal. (Football Insider)

Tottenham wanatarajiwa kupigana vikumbo na mahasimu wao wa London Kaskazini Arsenal katika mbio za kujaribu kumsajili beki wa Crystal Palace na England Marc Guehi, 22. (Evening Standard).

Bayern Munich wako tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya mshambuliaji wa Senegal Sadio Mane, 31, ambaye alijiunga nao akitokea Liverpool msimu uliopita wa joto. (90Min)

Fulham wanapanga kufanya mazungumzo na Leeds United kuhusu kumpa mkataba wa kudumu winga Muingereza Dan James, 25. (Football Insider)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’