Yanga - Local

Yanga katika mtego wa Singida BS

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 May 2023
Yanga katika mtego wa Singida BS

Kikosi cha Yanga kiliwasili mkoani Singida jana na jioni kuanza maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida BS ambao utapigwa Alhamisi, May 04 katika uwanja wa LITI

Meneja wa timu hiyo Walter Harrison amesema wametua Singida wakiwa na dhamira moja tu, kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

Yanga inaongoza Ligi ikiwa na alama 68, alama tano zaidi ya wapinzani wao Simba wanaoshika nafasi ya pili wakiwa na alama 63

Leo Simba inachuana na Namungo Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Majaliwa ambapo kama Simba watafanikiwa kuondoka na alama zote tatu watapunguza gap la pointi kutoka tano na kuwa mbili na kusalia mechi tatu

Lakini kama Yanga itashinda dhidi ya Singida BS itarejesha alama tano kileleni huku zikisalia mechi tatu za kuhitimisha msimu ambayo Wananchi watahitaji alama nyingine tano kutoka kwenye mechi hizo ili kuwa mabingwa

"Kikosi kimewasili salama Singida, jioni wachezaji walipata nafasi ya kufanya mazoezi ya kwanza hapa. Tutakamilisha mazoezi yetu ya mwisho kesho (leo) katika uwanja wa LITI"

"Tumekuja hapa kusaka ushindi ili tujiweke katika nafasi nzuri ya kutetea taji letu. Tunafahamu mechi hizi za mwishoni mwa msimu ni ngumu lakini tumekuja hapa kupambana kuhakikisha tunapata matokeo mazuri," alisema Walter

Baada ya mchezo wa nusu fainali ya kombe la FA kusogezwa mbele, Yanga itarejea jijini Dar es salaam baada ya mechi dhidi ya Singida BS ili kujiandaa na mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la CAF dhidi ya Malumo Galants ambao utapigwa Jumatano ijayo, May 10 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’