Baada ya kupoteza mchezo wa ligi kuu uliopita dhidi ya Prisons katika uwanja wao wa Nyankumbu, Geita Gold imepania kurejesha wimbi la ushindi katika mchezo unaofuata dhidi ya Mbeya City
Kocha msaidizi wa Geita Gold, Mathias Wandiba amesema hawakufurahishwa na kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Prisons na kwamba makosa yaliyojitokeza hawatarajii kujirudia kwenye mechi zilizobaki na kwamba hasira zote ni kwa Mbeya City
"Kwa ujumla matokeo hayo yalituumiza sana, ila haijirudii kwa sasa tunajipanga upya na mchezo ujao dhidi ya Mbeya City tukihitaji ushindi ili kuendelea kulinda nafasi yetu,” alisema Wandiba
Alisema wanaamini kwa maandalizi waliyonayo hawapoteza mchezo wowote ili kufikia malengo akiwaomba mashabiki kuendelea kuisapoti timu hiyo hadi mwisho wa ligi
Mchezo kati ya Geita Gold dhidi ya Mbeya City utapigwa May 13 katika uwanja wa Nyankumbu, Geita



