Unaweza kusema ni suala la muda tu Yanga kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya NBC kwa msimu wa pili mfululizo baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida BS katika mchezo uliopigwa uwanja wa Nafua LITI
Mabao ya Stephane Aziz Ki na Clement Mzize yalitosha kuihakikishia Yanga alama tatu muhimu ugenini
Wananchi waliuanza mchezo huo kwa kasi na walihitaji dakika 20 tu kujihakikishia alama tatu
Shuti la nje ya 18 kutoka kwa Aziz Ki kwenye dakika ya 15 lilimshinda mlinda lango Benwedict Haule kabla ya Mzize kufunga bao la pili kwenye dakika ya 20 akimalizia krosi ya Jesus Moloko
Yanga ilitengeneza nafasi nyingi zaidi kuliko wapinzani wao kwenye mchezo huo na pengine ilistahili kuondoka na ushindi mnono zaidi
Wananchi wamefikisha alama 71 wakijiimarisha kileleni kwa tofauti ya alama saba dhidi ya Simba inayoshika nafasi ya pili
Yanga inahitaji alama tatu tu kutoka mechi tatu ziilizobaki ili kutwaa ubingwa








