Msafara wa kikosi cha Simba unatarajiwa kuondoka Ruangwa leo kuelekea Mtwara kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Azam Fc
Mchezo huo utapigwa Jumapili, May 07 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona
Baada ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc, Simba iliweka kambi ya siku mbili Ruangwa mkoani Lindi
Mkakati wa Simba ni kuitafuta fainali ya kombe la FA, ili kuhakikisha msimu huu inatwaa angalau taji moja
Baada ya kupoteza matumaini kwenye ubingwa wa Ligi Kuu, Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira na benchi lake la ufundi wamepania kushinda taji la FA
Hata hivyo watalazimika kuifunga Azam Fc ambayo msimu huu imechukua alama nne mbele ya Simba katika mechi za Ligi