Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu May 08 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th May 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu May 08 2023

Barcelona wana uhakika wa kukamilisha dili ya kumsajili kiungo wa kati wa Manchester City na Ujerumani Ilkay Gundogan, 32. (90min)

Aston Villa wanajiandaa kumnunua fowadi wa Serbia Dusan Vlahovic, 23, kutoka Juventus . (Football Insider)

Tottenham wameitaka Barcelona kutaja bei yao kwa kiungo wa kati wa Ivory Coast Franck Kessie, 26. (Sport - in Spanish)

Liverpool haijawasiliana na Brighton kuhusu uhamisho wa kiungo wa kati wa Argentina Alexis Mac Allister, 24 (Athletic)

Rais wa Napoli Aurelio de Laurentiis anasema mabingwa hao wa Serie A hawatamuuza mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 24, ambaye amekuwa akihusishwa na baadhi ya vilabu vikubwa barani Ulaya, msimu huu wa joto.(Cinque Minuti, via Mail)

Nahodha wa zamani wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 33, ataondoka Chelsea - na anataka kurejea Barcelona . (Fabrizio Romano)

Aston Villa wako tayari kulipa dau la £60m la Fulham ili kumsajili kiungo wa kati wa Ureno Joao Palhinha, 27 kutoka klabu hiyo ya London(Football Insider)

Wakala wa mchezaji wa kimataifa wa Ureno Joao Cancelo amekutana na Barcelona kuhusu klabu hiyo kumsajili beki huyo wa Manchester City , ambaye yuko kwa mkopo Bayern Munich, kwa mkopo wa msimu mzima kukiwa na chaguo la kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. (Sport - in Spanish)

Manchester City wataangalia uwezekano wa kumnunua kiungo wa kati wa Bayern Munich Mholanzi Ryan Gravenberch, 20, ambaye amekuwa akihusishwa na Liverpool, iwapo watakosa kumnunua kiungo wa kati wa Uingereza Jude Bellingham, 19, kutoka Borussia Dortmund. (Mirror)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.