Real Madrid - International

Hazard kumaliza mkataba Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 May 2023
Hazard kumaliza mkataba Real Madrid

Eden Hazard amefichua kuwa hana nia ya kuondoka Real Madrid kabla ya mkataba wake kukamilika 2024

Hazard alikua mchezaji ghali zaidi wa Real Madrid alipojiunga na wababe hao wa La Liga kutoka Chelsea kwa ada ya pauni milioni 130 mwaka 2019

Lakini tangu kuwasili kwake katika mji mkuu wa Uhispania, Hazard amekuwa na wakati mgumu katika ubora na utimamu wa mwili na amekuwa kivuli cha mchezaji huyo aliyejizolea umaarufu mkubwa Stamford Bridge

Ameanza ligi mara moja tu msimu huu na alikuwa mbadala katika ushindi wa 2-1 wa Copa del Rey dhidi ya Osasuna Jumamosi jioni

Mbelgiji huyo anakubali kwamba msimu wake haukuwa mzuri lakini alithibitisha kuwa anapanga kumaliza kandarasi yake Santiago Bernabeu

"Umekuwa mwaka mgumu," Hazard mwenye umri wa miaka 32 aliiambia Cadena SER, kwenye Daily Mail

"Kusema kweli, ninapanga kusalia Real Madrid msimu ujao. Natarajia kubaki kwani nataka kusherehekea mwaka wa mwisho wa mkataba ambao nimebakisha"

"Nina uhusiano mzuri na klabu na wachezaji pia. Nataka kucheza, lakini najua ni ngumu sana. Lazima nifanye kazi na natumai naweza kucheza zaidi," alisema Hazard

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
2h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
3h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
3h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
6h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
10h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
11h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
11h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
12h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
12h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
13h ago
READ MORE β†’