Zilikuwa dakika dakika 90 za kibabe kwenye uwanja wa Bernabeu, Real Madrid na Manchester City wanatoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya
Ilikuwa ni mechi ya vipindi viwili. Manchester City walimiliki mpira mwingi zaidi katika kipindi cha kwanza. Kuanzia dakika ya kwanza, walishambulia zaidi, na kujaribu kuibana Real Madrid kwenye nusu yao.
Hata hivyo ni Real Madrid waliotangulia kufunga kwenye dakika ya 36 kupitia kwa Vinicious Junior aliyepiga shuti kali nje ya 18 baada ya pasi kutoka kwa Eduardo Camavinga
Real Madrid ilikwenda mapumziko ikiwa na uongozi wa bao 1-0 na ikarejea kipindi cha pili ikiwa na kasi ileile wakisaka bao la ushindi
Manchester City wakajibu kwenye dakika ya 67 Calvin De Bruyne aliyekuwa nyota wa mchezo huo akaifungia bao akipiga shuti kutoka nje ya 18 kama alivyofanya Vini Jr
Sare hiyo inaufanya mchezo wa mkondo wa pili ambao utapigwa Etihad kuwa nafasi sawa kwa kila timu pamoja na kwamba City wanaweza kuwa na nafasi kubwa zaidi katika uwanja wa nyumbani
Hata hivyo msimu huu Real Madrid wamedhihirisha wanaweza kupata ushindi katika uwanja wowote iwe nyumbani au ugenini



