Real Madrid - Manchester City - International

Real Madrid, Manchester City zatoshana nguvu UEFA CL

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 May 2023
Real Madrid, Manchester City zatoshana nguvu UEFA CL

Zilikuwa dakika dakika 90 za kibabe kwenye uwanja wa Bernabeu, Real Madrid na Manchester City wanatoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya

Ilikuwa ni mechi ya vipindi viwili. Manchester City walimiliki mpira mwingi zaidi katika kipindi cha kwanza. Kuanzia dakika ya kwanza, walishambulia zaidi, na kujaribu kuibana Real Madrid kwenye nusu yao. 

Hata hivyo ni Real Madrid waliotangulia kufunga kwenye dakika ya 36 kupitia kwa Vinicious Junior aliyepiga shuti kali nje ya 18 baada ya pasi kutoka kwa Eduardo Camavinga

Real Madrid ilikwenda mapumziko ikiwa na uongozi wa bao 1-0 na ikarejea kipindi cha pili ikiwa na kasi ileile wakisaka bao la ushindi

Manchester City wakajibu kwenye dakika ya 67 Calvin De Bruyne aliyekuwa nyota wa mchezo huo akaifungia bao akipiga shuti kutoka nje ya 18 kama alivyofanya Vini Jr

Sare hiyo inaufanya mchezo wa mkondo wa pili ambao utapigwa Etihad kuwa nafasi sawa kwa kila timu pamoja na kwamba City wanaweza kuwa na nafasi kubwa zaidi katika uwanja wa nyumbani

Hata hivyo msimu huu Real Madrid wamedhihirisha wanaweza kupata ushindi katika uwanja wowote iwe nyumbani au ugenini

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
8h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
15h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’