Wakati msimu wa mashindano 2022/23 ukiwa unaelekea ukingoni, Mtendaji Mkuu wa Simba Imani Kajula amesema wanatarajia kufanya maboresho makubwa ya kikosi ili kuhakikisha msimu ujao Simba inaweza kutimiza malengo yake katika mashindano yote ambayo itashiriki
Msimu ujao Simba itashiriki Ligi Kuu, FA Cup, Ligi ya Mabingwa na Super Ligi inayotarajiwa kuanza mwezi Oktoba 2023
Imeelezwa tayari kocha mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amewasilisha mapendekezo ya wachezaji ambao anawahitaji katika kikosi chake pamoja na orodha ya wachezaji ambao hawako katika mpango wake
Wachezaji ambao huenda wasiwe sehemu ya kikosi cha Simba msimu ujao ni pamoja na Joash Onyango, Nassoro Kapama, Habib Kyombo, Mohammed Ouattara, Jimmyson Mwanuke, na Augustine Okrah
Wengine ni Nelson Okwa, Ismail Sawadogo na Victor Akpan, huku Erasto Nyoni na Peter Banda wakiwa kwenye hatihati
Aidha chanzo kutoka ndani ya uongozi wa Simba kimedokeza wachezaji ambao wako kwenye mpango wa Simba ni pamoja na kiungo mshambuliaji wa Vipers Fc Milton Karisa
Wengine ni beki wa kati wa Rayon Sports ya Rwanda, Abdul Rwatubyaye, kiungo wa Geita Gold, Edmund John na kipa wa Vipers FC ya Uganda, Alfred Mudekereza
Robertinho ameuagiza uongozi wa Simba kukamilisha michakato ya usajili mapema ili timu itakapokwenda pre-season awe na wachezaji wote atakaowatumia msimu ujao



