Yanga yaichapa Marumo 2-0, yanusa fainali

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th May 2023


Yanga yaichapa Marumo 2-0, yanusa fainali

Bado dakika 90 kwa Yanga kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Marumo Gallants katika mchezo wa nusu fainali mkondo wa kwanza

Wakicheza kwa nidhamu kubwa vijana Nasreddine Nabi walihitaji dakika 30 za mwisho kuibuka na ushindi huo mnono kwa mabao ya Stephane Aziz Ki na Bernard Morrison

Aziz Ki alifunga bao la kwanza kwenye dakika ya 64 akimalizia pasi murua kutoka kwa Tuisila Kisinda

Baada ya kuingia kwa bao hilo Marumo Gallants waliokuwa bora katika kipindi cha pili, waliongeza kasi kusaka bao la kusawazisha lakini ilikuwa kama mtego kwao

Shambulizi la kushitukiza dakika za majeruhi likamshuhudia Morrison akifunga bao la pili baada ya pasi kutoka kwa Fiston Mayele

Ulikuwa mchezo mgumu lakini Yanga imefanikiwa kuondoka na ushindi muhimu ambao wataenda nao Afrika Kusini wakiwa na faida ya mabao mawili nyumbani

Ni dakika 90 tu zimebaki kwa Yanga kuweka rekodi ya kutinga fainali ya kombe la Shirikisho


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.