Yanga - Local

Yanga yaichapa Marumo 2-0, yanusa fainali

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 May 2023
Yanga yaichapa Marumo 2-0, yanusa fainali

Bado dakika 90 kwa Yanga kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Marumo Gallants katika mchezo wa nusu fainali mkondo wa kwanza

Wakicheza kwa nidhamu kubwa vijana Nasreddine Nabi walihitaji dakika 30 za mwisho kuibuka na ushindi huo mnono kwa mabao ya Stephane Aziz Ki na Bernard Morrison

Aziz Ki alifunga bao la kwanza kwenye dakika ya 64 akimalizia pasi murua kutoka kwa Tuisila Kisinda

Baada ya kuingia kwa bao hilo Marumo Gallants waliokuwa bora katika kipindi cha pili, waliongeza kasi kusaka bao la kusawazisha lakini ilikuwa kama mtego kwao

Shambulizi la kushitukiza dakika za majeruhi likamshuhudia Morrison akifunga bao la pili baada ya pasi kutoka kwa Fiston Mayele

Ulikuwa mchezo mgumu lakini Yanga imefanikiwa kuondoka na ushindi muhimu ambao wataenda nao Afrika Kusini wakiwa na faida ya mabao mawili nyumbani

Ni dakika 90 tu zimebaki kwa Yanga kuweka rekodi ya kutinga fainali ya kombe la Shirikisho

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’