Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi May 11 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 May 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi May 11 2023

Kipa wa Tottenham na Ufaransa Hugo Lloris, 36, ana ofa ya kucheza Saudi Arabia msimu ujao kwa mshahara ambao ni mara tatu ya ule anaopokea sasa katika klabu ya Spurs. (Times - usajili unahitajika)

Newcastle wamefufua nia yao ya kumnunua kiungo wa Leicester mwenye umri wa miaka 26 James Maddison. (Telegraph - usajili unahitajika)

Liverpool wana nia ya kumsajili kiungo wa Real Madrid na Ufaransa Aurelien Tchouameni, 23, walau kwa mkataba wa mkopo. (90 Min)

Tottenham wanamtafu atakayechukua nafasi ya mkurugenzi mkuu wa zamani Fabio Paratici kabla ya kukamilisha mipango ya kumsajili kocha mpya. (Mirror)

Manchester City wameelekeza darubini yao kwa kiungo wa kati wa Chelsea na Croatia Mateo Kovacic mwenye umri wa miaka 29 kama mbadala wa kiungo wa kati wa Uingereza Jude Bellingham, 19, ambaye anatazamiwa kujiunga na Real Madrid kutoka Borussia Dortmund. (Football Insider)

Liverpool wako tayari kumsajili mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ujerumani na klabu ya Hannover 96, Ron-Robert Zieler, 34 kama kipa wa ziada (Bild - kwa Kijerumani)

Napoli wameongeza bei ya Victor Osimhen hadi euro milioni 160 wakitarajia kinyang'anyiro kikali baina ya vilabu vinavyomwania mshambuliaji huyo wa Nigeria mwenye umri wa miaka 24. (Il Matino - kwa Kiitaliano)

Mshambulizi wa AC Milan na Ureno Rafael Leao, 23, ambaye amekuwa akihusishwa na Liverpool na Chelsea, amesaini mkataba mpya wa miaka mitano na klabu hiyo ya Italia. (Athletic- Usajili unahitajika)

Manchester United inamfuatilia mshambuliaji wa Inter Milan na Argentina Lautaro Martinez, 25. (Football Insider)

Kipa wa Uingereza Aaron Ramsdale, 24, anakaribia kuafiki mkataba mpya wa muda mrefu Arsenal. (ESPN)

Sunderland wanapanga kumpa Jack Clarke kandarasi mpya ili kusambaratisha nia ya Crystal Palace na Brentford kumnunua mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 22. (TeamTalk)

Mshambuliaji wa Barcelona Mbrazil Raphinha, 26, ambaye amekuwa akihusishwa na Newcastle, amekanusha madai kuwa yuko tayari kuondoka Nou Camp msimu huu wa joto. (Chronicle Live)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’