Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Marumo Gallants jana katika mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho barani Afrika mkondo wa kwanza, Yanga imevuna Tsh Milioni 20 kutoka kwa bonas ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan
Rais aliongeza dau kutoka Milioni 5 kuwa Milioni 10 kuanzia hatua ya nusu fainali ambayo Yanga ilifanikiwa kufuzu huku watani zao Simba wakiondoshwa hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa
Sasa Yanga imevuna jumla ya Tsh Milioni 70 za bonas kutoka mabao 12 waliyofunga kuanzia hatua ya makundi

