Yanga yapania kutangaza ubingwa mbele ya Dodoma Jiji

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th May 2023


Yanga yapania kutangaza ubingwa mbele ya Dodoma Jiji

Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema wanahitaji kupambana kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa uwanja wa Azam Complex hapo kesho ili kuhakikisha wanashinda na kutwaa ubingwa

Nabi amesema anawaheshimu Dodoma Jiji ni timu nzuri lakini muhimu kwa timu yake ni alama tatu ambazo zitawahakikishia ubingwa

"Tumetoka kucheza mchezo wa kwanza wa nusu fainali kombe la Shirikisho, yapo mapungufu tuliyaona katika mchezo huo ambayo tumeyafanyia kazi"

"Japo tuna changamoto ya uchovu na majeraha kwa baadhi ya wachezaji, lakini nina imani na wachezaji wangu wale watakaopata nafasi kesho watapambana kutupatia ushindi"

"Nawaheshimu Dodoma Jiji ni timu nzuri lakini sisi malengo yetu ni kutafuta ushindi ili tuweze kuwa mabingwa," alisema Nabi

Nae mshambuliaji kinara wa mabao Fiston Mayele amesema kwa upande wa wachezaji mawazo yao ni kushinda mchezo dhidi ya Dodoma Jiji ili wawe mabingwa

Akiwa kiongozi kwenye safu ya ushambuliaji, Mayele amewaahidi Wananchi kuwa kama atapewa nafasi ya kucheza mchezo huo, atapambana ili awape furaha

"Sisi wachezaji tuko tayari kwa mchezo dhidi ya Dodoma Jiji, tumeshasahau furaha ya ushindi wa juzi. Binafsi kama nitapewa nafasi ya kucheza hapo kesho nitahakikisha napambana ili niwape furaha mashabiki wa Yanga," alisema Mayele


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.