KMC yaichapa Singida BS 2-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th May 2023


KMC yaichapa Singida BS 2-0

KMC imejiondoa katika eneo la hatari kwenye msimamo wa ligi kuu ya NBC baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida BS katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru

Mabao ya Daruweshi Saliboko na Cliff Buyoya yameihakikishia KMC alama tatu muhimu na hivyo kufikisha alama 29 na kusogea mpaka nafasi ya 12

Ulikuwa ushindi wa kwanza kwa kocha Jamhuri Kiwhelo 'Julio' ambaye KMC walimpa mission ya kuinusuru timu hiyo kuteremka daraja

KMC imesalia na mechi mbili za kuhitimisha msimu ambapo wanahitaji angalau alama tatu ili kujihakikishia kutoshuka daraja moja kwa moja ingawa wanaweza kuingia eneo la play-off


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.