KMC imejiondoa katika eneo la hatari kwenye msimamo wa ligi kuu ya NBC baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida BS katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru
Mabao ya Daruweshi Saliboko na Cliff Buyoya yameihakikishia KMC alama tatu muhimu na hivyo kufikisha alama 29 na kusogea mpaka nafasi ya 12
Ulikuwa ushindi wa kwanza kwa kocha Jamhuri Kiwhelo 'Julio' ambaye KMC walimpa mission ya kuinusuru timu hiyo kuteremka daraja
KMC imesalia na mechi mbili za kuhitimisha msimu ambapo wanahitaji angalau alama tatu ili kujihakikishia kutoshuka daraja moja kwa moja ingawa wanaweza kuingia eneo la play-off



