Mbeya City yajitutumua mbele ya Geita Gold

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th May 2023


Mbeya City yajitutumua mbele ya Geita Gold

Mbeya City imeondoka kwenye eneo la play-off baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Geita Gold

Bao la George Sangija liliihakikishia Mbeya City kupata ushindi muhimu uwanja wa Nyankumbu huko Geita na kufikisha alama 30

Mbeya City wamepanda mpaka nafasi ya 12 wakiishusha KMC yenye alama 29 katika eneo la play-off

Ruvu Shooting imekuwa timu ya kwanza kushuka daraja huku Polisi Tanzania ikiwa katika hatari, alama 22 kwenye nafasi ya 15

Polisi Tanzania wanahitaji kushinda mechi zote tatu zilizobaki huku ikiomba wapinzani wake wasipate matokeo mazuri katika mechi zao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.