Simba - Local

Saido, Chama katika vita ya mchezaji bora wa msimu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 May 2023
Saido, Chama katika vita ya mchezaji bora wa msimu

Kitu pekee kinachowaumiza Wanasimba ni kuona wameshindwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu licha ya kuwa na kikosi bora sana msimu huu

Ukiangalia takwimu, Simba imeongoza katika kufunga na kutengeneza nafasi nyingi za mabao

Wachezaji Saido Ntibazonkiza na Clatous Chama wana nafasi kubwa katika kinyan'ganyiro cha tuzo ya mchezaji bora wa msimu huu

Saido ndiye mchezaji aliyehusika katika mabao mengi zaidi msimu huu akiwa na assist 12 na pia akifunga mabao 10 na jumla kuhusika katika mabao 22 akiwa na Simba na Geita Gold

Chama yeye ametoa assist 14 na kufunga mabao 4 na hivyo kuhusika katika mabao 18 akiwa sawa na mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele aliyefunga mabao 16 na kutoa assist 2

Ni wazi Saido na Chama wanaweza kuchuana katika kinyang'anyiro cha mchezaji bora wa msimu Saido akiwa na nafasi kubwa zaidi

Katika msimu huu Simba imefunga mabao 66 na kuruhusu mabao 15 wakiwa wamefunga mabao 10 zaidi ya watani zao Yanga waliofunga mabao 55 timu zote zikiruhusu mabao 15

Simba ndio timu pekee iliyofungwa mechi moja tu mpaka sasa msimu huu

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
3h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
3h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
7h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
11h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
12h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
13h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
14h ago
READ MORE β†’