Barcelona wameshinda La Liga kwa mara ya kwanza tangu 2019. Ushindi wao wa 4-2 dhidi ya wapinzani wao wa jiji Espanyol ulimhakikishia Xavi taji katika msimu wake wa kwanza kamili kama meneja wa klabu ambayo alishinda mataji manane ya ligi akiwa mchezaji
Real Madrid, ambao wanashika nafasi ya pili kwenye jedwali, waliilaza Getafe 1-0 Jumamosi na Atletico Madrid, katika nafasi ya tatu, kwa kushangaza walifungwa 1-0 na Elche mapema Jumapili kabla ya Barcelona kutwaa taji hilo kwa ushindi wa Espanyol
Mabao ya Robert Lewandowski, Alejandro Balde na Jules Kounde yalihitimisha ubingwa huo
Umekuwa msimu wa mchanganyiko kwa Barcelona - walitupwa nje ya Ligi ya Mabingwa katika hatua ya makundi na kisha wakatolewa kwenye Ligi ya Europa dhidi ya Manchester United - lakini wamefunga taji la kwanza la ligi ndani ya miaka minne
Hili ni taji la 27 la klabu hiyo ya La Liga, ambalo linawaacha wanane nyuma ya wapinzani wao - Real ambao wameshinda La Liga mara 35. Atletico wanashika nafasi ya tatu kwenye orodha hiyo, wakiwa wametajwa kuwa mabingwa mara 11