Yanga imeandika historia kwa kutinga fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho kibabe sana baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Marumo Gallants huko Afrika Kusini
Ni ushindi wa jumla wa mabao 4-1 baada ya ushindi wa mabao 2-0 nyumbani
Mabao ya Fiston Mayele na Kennedy Musonda yameihakikishia Yanga ushindi muhimu ugenini unaoipeleka fainali huku ikivunja rekodi ya Marumo kutofungwa katika uwanja wao wa nyumbani katika michuano hiyo
Yanga inamsubiri mshindi wa mchezo kati ya USM Alger dhidi ya Asec Mimosas



Wananchiiiiiiiiiii fainali hiyooooooooo..



