Yanga - Local

Ni Yanga vs USM Alger fainali CAF CC

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 May 2023
Ni Yanga vs USM Alger fainali CAF CC

Wananchi wana dakika 180 za kuwania ubingwa wa kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya ushindi wa jumla wa mabao 4-1 dhidi ya Marumo Gallants katika mchezo wa nusu fainali

Jana Yanga ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Marumo katika mchezo wa nusu fainali mkondo wa pili uliopigwa Afrika Kusini huku pia ikishinda mabao 2-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa wiki iliyopita

Yanga itachuana na USM Alger (USMA) katika hatua ya fainali baada ya Waarabu hao kutoka Algeria kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya ASEC Mimosas katika mchezo wa mkondo wa pili nusu fainali uliopigwa huko Algeria

Timu hizo zilitoka suluhu ya bila kufungana kwenye mchezo wa nusu fainali mkondo wa kwanza huko Ivory Coast

Fainali hii itakuwa kisasi kwa Yanga, Wananchi wakiwa na kumbukumbu ya timu hizo kukutana kwenye michuano hii hatua ya makundi mwaka 2018

USMA waliifunga Yanga 4-0 katika mchezo wa kwanza hatua ya makundi uliopigwa Algeria na Yanga kushinda 2-1 katika mchezo wa marudiano

Wakati huo Yanga ilikuwa ikinolewa na kocha Mwinyi Zahera aliyetua kuchukua nafasi ya George Lwandamina ambaye alirejea kunako klabu yake ya zamani Zesco United

Mchezo wa fainali mkondo wa kwanza utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa May 28 na marudiano kupigwa Algeria Juni 03

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’