Arsenal wanatayarisha ofa ya pauni milioni 92 kwa kiungo wa kati wa West Ham na Uingereza Declan Rice, 24, ambayo itakuwa uhamisho wa rekodi ya klabu kwa The Gunners. (Telegraph)
Bayern Munich pia wanavutiwa na Rice huku bosi wake Thomas Tuchel akitafuta kuimarisha safu yake ya kiungo. (Mirror)
Meneja wa Arsenal Mikel Arteta pia ana nia ya kumsajili beki wa pembeni wa Manchester City na Ureno Joao Cancelo, 28, ambaye kwa sasa yuko Bayern Munich kwa mkopo, lakini Arsenal wanahofia kuwa City watasita kufanya biashara nao msimu huu wa joto. (Sport)
Paris St-Germain wanataka kumsajili Bernardo Silva wa Manchester City, 28, baada ya kushindwa kumpata kiungo huyo wa kati wa Ureno msimu uliopita, huku ada ya hivi punde ikiaminika kuwa takriban £70m. (Telegraph)
Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp alitaka kumbakisha kiungo wa kati wa Uingereza James Milner, 37, na kumpa mkongwe huyo nafasi ya ukocha katika klabu hiyo. (Mirror)
Manchester United wamekubali makubaliano ya kibinafsi na beki wa Napoli mwenye umri wa miaka 26 Kim Min-jae. (Il Mattino, via Metro)
Kiungo wa kati wa Arsenal na Norway Martin Odegaard anatazamiwa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo, huku mkataba wa sasa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ukikamilika 2025. (90min)
Kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso amethibitisha kuwa bado ataendelea kuinoa klabu hiyo ya Ujerumani msimu ujao baada ya kiungo huyo wa zamani wa Liverpool kuhusishwa na nafasi ya meneja iliyo wazi ya Tottenham. (Sky Sports)
Mchezaji wa Arsenal Albert Sambi Lokonga, 23, anaweza kutaka kuhamia Burnley ili kuungana na meneja Vincent Kompany, ambaye alimfundisha Mbelgiji huyo katika klabu ya Anderlecht. (Express)
Mshambuliaji wa Ivory Coast Wilfried Zaha anafikiria kusalia Crystal Palace, huku kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 ikimalizika msimu huu wa joto. (Sports)
Barcelona watafanya jaribio jipya la kumnunua kiungo wa kati wa Real Sociedad na Uhispania Martin Zubimendi, 24, msimu huu baada ya Arsenal kuripotiwa kushindwa na ofa ya pauni milioni 53 mwezi Januari. (Express)
Mshambulizi wa Senegal Sadio Mane, 31, anataka kusalia Bayern Munich licha ya ugomvi wake na mchezaji mwenzake Leroy Sane mwezi Aprili. (Fabrizio Romano)
Meneja wa zamani wa Bayern Munich Julian Nagelsmann alikuwa chaguo la kwanza la Chelsea kuchukua nafasi ya Graham Potter, kulingana na wakala wa Mjerumani huyo. (The Times – Subscription is needed)
BBC



