Manula kutibiwa Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th May 2023


Manula kutibiwa Afrika Kusini

Mlinda lango namba moja wa Simba na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Aishi Manula anatarajiwa kupelekwa Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi baada ya kuumia akiwa kwenye majukumu na klabu yake

Manula aliumia kwenye mchezo wa robo fainali kombe la FA dhidi ya Ihefu Fc, mchezo ambao Simba ilishinda mabao 5-0

Meneja wa Manula Jemedari Said amesema bado mchezaji huyo anauguza jeraha na klabu ya Simba inajiandaa kumpeleka Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi 

"Mchezaji ni wa klabu kwa hiyo mwenye jukumu la kumtibu ni klabu yake ya Simba. Tayari taratibu zimeshafanyika na muda si mrefu atapelekwa kwenye matibabu wiki hii"

"Amepelekwa Muhimbili, ikaonekana kuna damu imevuja kwa ndani na madaktari wakabaini msuli umekatika kwa hiyo anahitaji upasuaji ambapo utafanyika nje ya nchi," alisema Jemedari


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.