Serikali ya Brazil imetoa tamko la kutokubaliana na vitendo vya ubaguzi wa rangi alichofanyiwa raia wake Vinicius Jr wakati wa mchezo wa kipigo cha 1-0 cha Real Madrid dhidi ya Valencia katika dimba la Mestalla siku ha Jumapili
Taarifa iliyotolewa na Serikali ya Brazil, imelaani matukio hayo yanayojirudia mara kwa mara kwa Vini Jr na kutaka yakomeshwe
"Tunakataa uchokozi mwingine wa ubaguzi wa rangi dhidi ya Vini Jr. Tutaitaarifu mamlaka ya Uhispania na La Liga kuwa Serikali ya Brazil haitavumilia ubaguzi wa rangi hapa au nje. Tutafanya kazi ili kila mwanamichezo mweusi aweze kucheza bila kukumbana na hili." imesema Serikali ya Brazil



