Juventus - International

Juventus yapokwa alama 10 Serie A

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 May 2023
Juventus yapokwa alama 10 Serie A

Klabu ya Juventus imepata mapigo mawili usiku wa Jumatatu; kipigo cha 4-1 dhidi ya Empoli kwenye mchezo wao wa Serie A na lingine ni kukatwa alama 10 kufuatia uchunguzi wa mwaka mzima wa mikataba isiyofaa ya uhamisho

Mapema msimu huu Kibibi Kizee hicho cha Turin kilipokwa alama 15 kwa makosa ya kifedha na kutoa hesabu za uongo juu ya mikataba ya uhamisho hukumu ambayo ilienda sambamba na kusimamishwa baadhi ya viongozi wake wa zamani

Hata hivyo ilikata rufaa na kurejeshewa alama zote 15. Hukumu mpya imetangazwa Jumatatu Mei 22 ambapo safari hii Juventus wamepokwa alama 10 na kushuhudiwa ikiporomoka kwenye msimamo wa Serie A kutoka nafasi ya pili alama 69 mpaka nafasi ya 7 alama 59

Tofauti na kashfa ya 'Calciopoli', ambayo ilishuhudia Juventus wakishushwa daraja na kupokonywa mataji mawili ya Serie A mnamo 2006, hukumu hii ya sasa inahusiana makosa ya kifedha na ‘Plusvalenza’ (hesabu za uongo juu ya mikataba ya uhamisho)  kimsingi ni kunufaika kutokana na mauzo ya mchezaji kutoka klabu moja hadi nyingine bila kufichua hesabu sahihi

Klabu ya AC imenufaika na maswaibu hayo ya Juventus katika mbio za kuwania kumaliza katika nafasi nne za juu. AC Milan ambayo weekend hii itachuana na Juventus wataingia katika mchezo huo wakiwa wamesogea mpaka nafasi ya nne kwenye jedwali la Serie A.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’