Kocha wa zamani wa Al Ahly Pitso Mosimane ameiongoza klabu yake ya Al Ahli Saudi kutwaa ubingwa wa Ligi daraja la kwanza Nchini Saudi Arabia kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Al-Qadisiyah FC
Ushindi huo umeifanya Al Ahli kufikisha pointi 71 kwenye msimamo wa ligi na kujihakikishia ubingwa baada ya wapinzani wake karibu Al Akhdood (alama 65) kupokea kichapo cha 3-2 dhidi ya Al Sahel SC na kuporomoka mpaka nafasi ya tatu huku Al Hazem FC (alama 67) ikikwea mpaka nafasi ya pili
Mosimane aliichukua Al Ahli ikiwa nafasi ya tano na kuiongoza kushinda mechi 18, sare 6 na vipigo vitatu na kuipandisha daraja kwenda Ligi kuu ya Saudi Pro sambamba na kutwaa ubingwa huo wa kihistoria
Mosimane ametwaa kombe lake la 19 katika maisha yake ya ukocha likiwa ni kombe lake la kwanza akiwa nje ya Afrika.



