Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi May 25 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 May 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi May 25 2023

Manchester United hawana budi kulipa pauni milioni 140 kama wanataka kumsajili mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, msimu huu baada ya kuafikiana dili la mchezaji-mwenza na mlinzi wa Korea Kusini Kim Min-jae, 26. (Il Mattino) via Mirror)

Napoli wanajaribu sana kumshawishi Kim kusaini mkataba mpya kabla ya kifungu cha kuachiliwa kuanza kutumika msimu huu wa joto. (90 Min)

Mikel Arteta yuko tayari kumruhusu kiungo wa kati wa Uingereza Emile Smith Rowe, 22, kuondoka Emirates ili kutoa nafasi kwa kiungo wa Leicester na England James Maddison, 26. (Mirror)

The Gunners pia wana nia ya kumuongeza mshambuliaji wa Torino na Paraguay Antonio Sanabria, 26, kwa mkataba wa thamani ya £21.6m. (La Repubblica via Mail)

Mshambulzi wa Tottenham na England Harry Kane, 29, bado anasalia kuwa chaguo la kwanza la Manchester United na klabu hiyo inapania kuanza mapema kufanya mazungumzo na Spurs. (Guardian)

Real Betis huenda ikafufua nia yao ya kumnunua kiungo wa kati wa Leeds United Mhispania Marc Roca, 26, ikiwa klabu hiyo ya Yorkshire itashushwa daraja kutoka Ligi ya Premia. (Estadio Deportivo)

Arsenal wamempa kiungo wa Uingereza Reiss Nelson mkataba mpya hadi 2027, inayojumuisha chaguo la nyongeza ya mwaka, lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 pia amepokea ofa kutoka kwa timu zingine za Ligi ya Premia, Italia na Uhispania. (Fabrizio Romano)

Kocha wa Swansea, Russell Martin amekubali kuwa meneja mpya wa Southampton. (Sky Sports)

Martin, 37, amekubali mkataba wa miaka mitatu kuwa meneja mpya wa Southampton, huku klabu hiyo iliyoshuka daraja ya Premier League ikitarajiwa kutangaza kuteuliwa kwake siku zijazo. (Sun)

Barcelona wameshangazwa na tetesi kwamba mlinzi wa Ufaransa Jules Kounde, 24, anataka kuondoka katika klabu hiyo, mwaka mmoja tu baada ya kujiunga nayo kutoka Sevilla. (90 Min)

Manchester United wako tayari kulipa pauni milioni 55 kumnunua kiungo wa Chelsea na England Mason Mount na nia yao kuzishinda Liverpool na Arsenal katika mbio za kuinasa saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Mail)

Mount atajadili mustakabali wake wa Chelsea katika mkutano na uongozi wa klabu hiyo wiki ijayo. (90 Min)

Mount ataelekea Manchester United ikiwa Chelsea itaamua kumuuza. (The Atheletic- Usajili unahitajika)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’