Polisi - Simba - Azam - Local

Polisi Tanzania yazipania Simba, Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 May 2023
Polisi Tanzania yazipania Simba, Azam Fc

Huku ikiwa katika hatari ya kushuka daraja, Polisi Tanzania imesema itapambana kwa 'jasho na damu' kuhakikisha inavuna pointi sita katika mechi zake mbili zilizobakia za Ligi Kuu Tanzania Bara, imefahamika

Polisi Tanzania imebakisha mechi mbili zote za ugenini ambazo ni dhidi ya Simba na Azam FC, zote za Dar es Salaam.

Maafande hao wako katika nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mkononi wana pointi 25, wakiwa mbele ya Ruvu Shooting yenye pointi 20 ambayo inaburuza mkia na rasmi imeshashuka daraja.

Afisa Habari wa Polisi Tanzania, Frank Lukwalo, alisema timu yao haijakata tamaa na imejipanga kuonyesha soka la burudani katika mechi zilizobakia ili malengo yao ya kupata ushindi yatimie.

Lukwalo alisema wachezaji wao watacheza kwa tahadhari kwa sababu wanahitaji kupata ushindi katika mechi zao bila kujali matokeo ya michezo mingine yatakavyokuwa.

"Tumejipanga kutumia kauli mbiu yetu ya machozi, jasho na damu, ili kuhakikisha tunavuna alama sita zitakazotuwezesha kubaki katika Ligi Kuu Bara"

"Mwalimu Zahera (Mwinyi), anaendelea na mikakati yake ya kukisuka vyema kikosi ili tupate ushindi kwenye mechi zetu mbili zilizobakia dhidi ya Simba na Azam FC"

"Mikakati bado inaenda vizuri katika mechi hizi zilizobakia tufanye vizuri, hatujakata tamaa hadi sasa na hakuna mchezaji yoyote aliyekata tamaa hadi mwisho wa ligi, hali ya kikosi ipo vizuri kuelekea michezo hiyo," alisema Lukwalo

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
8h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
9h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’