Baada ya kukwama Yanga, Feisal aomba michango aende CAS

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th May 2023


Baada ya kukwama Yanga, Feisal aomba michango aende CAS

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Feisal Salum ameomba watanzania na wapenzi wa soka kumchangia fedha ili aende Mahakama ya Usuluhishi ya Kimataifa ya michezo CAS

Feisal ametumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii akiomba Watanzania wamuwezeshe kifedha ili aweze kumudu gharama za kufungua kesi CAS katika dhamira yake ya kuruhusiwa kuvunja mkataba wake na Yanga

"Ndugu zangu Watanzania na familia yote ya soka kwa Bara na visiwani. Mimi kijana wenu ambaye kwa miaka yote nimekua na nidhamu nje na ndani ya uwanja na kwa dhati nimeitumikia klabu ya Yanga na Timu ya Taifa ya Tanzania na Zanzibar Heros:

"Utiifu wangu umekua shubiri ya maisha yangu ya soka, nimevumilia nimeshindwa, sitamani tena mama yangu kutukanwa. TFF imeshindwa kunisaidia kupata haki yangu ya Kuvunja mkataba na Yanga hivyo nimeamua Kwenda Mahakama ya michezo CAS:

"Nahitaji Mchango wa kila Mtanzania mpenda haki na maendeleo ya wachezaji wa Kitanzania ambao wamekua kimya na woga juu ya maslahi, Heshima na Haki zao. Naomba unichangie kadiri utakavyoweza ili niweze kupata pesa ya Kulipia gharama za kufungua Jalada la kesi yangu CAS ili kupata Haki yangu ya Kuondoka Yanga kwa kuvunja mkataba," aliandika Feisal

Gharama ya kufungua kesi CAS inakadiriwa kufikia Tsh Milioni 56


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.