Real Madrid wako tayari kutangaza hatua yao ya kusaini mkataba ya kiungo wa kati wa England Jude Bellingham, 19, kutoka Borussia Dortmund wiki ijayo. (Marca - in Spanish)
Kiungo wa kati wa West Ham na England Declan Rice angependelea kujiunga na Arsenal msimu huu, huku Manchester United, Chelsea na Bayern Munich pia wakiwa na nia na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Mirror)
Manchester United bado hawakidhi kiwango cha Chelsea cha £55m ambayo ndio thamani waliyompa kiungo wa kati wa England Mason Mount licha ya kuongoza mbio za kinyang’anyiro cha kumchukua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka . (Independent)
Chelsea wanaangalia jinsi ya kumuuza mmoja wa walindalango wao wawili, huku mchezaji wa kimataifa wa Senegal Edouard Mendy, 31, akiwa na uwezekano mkubwa wa kuondoka katika klabu hiyo msimu huu . (90min)
Newcastle wamewatuma waangalizi wao kumfuatilia kwa karibu kiungo wa safu ya kati wa RB Leipzig na Hungary Dominik Szoboszlai, 22, mara mbili katika kipindi cha wiki mbili . (Sky Sports)
Manchester City wako tayari kutoka kitita cha euro milioni 40 (£35m) zinazohitajika kama garama ya kumnunua beki wa Ureno Joao Cancelo, ambaye kwa sasa anacheza kwa mkopo katika Bayern Munich, huku Barcelona pia wakiwa na nia na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. (Sport - in Spanish)
City wanajiandaa kumtumia Cancelo katika mkataba wa kubadilishana wachezaji na kiungo wa kati wa Bayern na Ujerumani Joshua Kimmich, 28. (90min)
Marco Asensio yuko tayari kuondoka Real Madrid wakati mkataba wake utakapokamilika mwishoni mwa msimu huu baada ya mazungumzo baina ya klabu hiyo na kiungo huyo wa kati wa Uhispania mwenye umri wa miaka 27, kugonga mwamba. (Athletic - subscription required)
Asensio yuko katika mazungumzo ambayo yamefikia kiwango cha kukaribia kujiunga na Paris St-Germain kama wakala huru. (ESPN)
Tottenham wanaongoza katika mbio za kununua mlindalango wa Brentford na Uhispania David Raya, 27. (GiveMesport)
Mlindalango wa SC Freiburg na Netherlands Mark Flekken anakaribia kabisa kusaini mkataba kwa ajili ya kujiunga na Brentford, huku klabu hiyo ya Primia Ligi ikiwa tayari kurefusha mkataba na kijana huyo mwenye umri wa miaka 29-wenye kipengele cha thamani ya €13m (£10.4m) cha kumuachilia. (Sky Sports Germany)
Leeds United huenda wasisaini mkataba wa kudumu msimu huu na kiungo wa kati wa United States Weston McKennie, 24, wakati mkataba wake wa mkopo utakapoisha katika Juventus . (Calciomercato - in Italian)
West Ham wwanamtaka beki wa Arsenal Mreno Nuno Tavares, 23, ambaye kwa sasa anacheza kwa mkopo katika klabu ya Marseille. (Record - in Portuguese)
Winga wa Arsenal mwenye umri wa miaka 23-Muingereza Reiss Nelson yuko tayari kuafiki mkataba wa muda mrefu na klabu hiyo. (Athletic - subscription required) Tottenham wako tayari kusikiliza ofa ya mlinzi wa Wales are willing to listen to offers mwenye umri wa miaka 30, Ben Davies msimu huu. (Football Insider)
BBC