Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema ana furaha kufanya kazi na Simba, matumaini yake ni kuwa atawasaidia wekundu hao wa Msimbazi kushinda mataji
Robertinho amesema amepata sapoti kubwa kutoka kwa uongozi wa Simba anafurahia sapoti ya mashabiki vile wanavyoiunga mkono timu yao
Licha ya kutokuwa na msimu wa mafanikio, Kocha huyo raia wa Brazil, amesema alifanya uamuzi sahihi kujiunga na Simba
"Nikiwa na Vipers Fc baada ya kuitoa TP Mazembe kwenye ligi ya mabingwa, nilipata ofa nyingi sana lakini nikachagua kuja Simba. Nilizungumza na viongozi na kwa kweli naipenda Simba, nawapenda Watanzania, mashabiki wanapenda sana soka na wanazipenda timu zao"
"Simba ni klabu kubwa hapa Afrika na hata duniani, kuna vitu tunapaswa kufanya ili tuweze kuonyesha ukubwa wetu. Tutakuwa na nafasi nzuri ya kufanya maboresho pale ligi itakapomalizika," alisema Robertinho
Simba itakamilisha msimu kwa mechi mbili dhidi ya Polisi Tanzania (Juni 06) na Coastal Union (Juni 09)



