Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu, May 29 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th May 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu, May 29 2023

Barcelona wanataka kumsajili kiungo wa kati wa Brazil Bruno Guimaraes, lakini klabu hiyo inaamini itapaswa kutoa ada ya uhamisho ya takriban euro milioni 100 (£87m) ili kuwashawishi Newcastle United kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Times)

Real Madrid wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino, 31, ambaye atakuwa mchezaji huru mkataba wake na Liverpool utakapokamilika msimu huu wa joto. (Fabrizio Romano)

Meneja wa zamani wa Tottenham na Paris St-Germain Mauricio Pochettino, 51, ametia saini mkataba wa miaka mitatu kuwa kocha mkuu mpya wa Chelsea. (Guardian)

Brazil bado wana matumaini ya kumshawishi kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti kuwa kocha wao mkuu ajaye. Mabingwa hao mara tano wa dunia wamekuwa bila kocha tangu Tite alipoondoka mara baada ya fainali za Kombe la Dunia huko Qatar mwezi Disemba. (Athletic)

Liverpool wanaweza kumsajili kiungo wa Lazio Sergej Milinkovic-Savic, 28, kwa euro 26m (£22.5m), huku mkataba wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Serbia ukitarajia kumalizika 2024. (Calciomercato via Goal)

Matumaini ya Manchester United kumsajili beki wa Korea Kusini Kim Min-jae, 26, na mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 24, kutoka Napoli yameongezeka huku kukiwa na uvumi kuhusu mustakabali wa meneja wa timu hiyo ya Italia Luciano Spalletti. (Givemesport)

Newcastle United pia wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kutaka kumsajili Kim wa Napoli. (Fijaches)

Sheffield United inamfuatilia kiungo wa kati wa Nottingham Forest Muingereza Lewis O'Brien, 24, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo DC United. (Sun)

Crystal Palace wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa kati wa Bournemouth na Colombia Jefferson Lerma, 28, kwa uhamisho huru (wa bure) msimu huu wa joto. (Fabrizio Romano)

Mshambuliaji na mchezaji aliye huru wa Chile Alexis Sanchez, 34, anatamani tena kurejea katika Ligi kuu ya England - baada ya kuzichezea Arsenal na Manchester United – wakati huu akimaliza mkataba wake Marseille. (Sun)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.