Pazia la Ligi kuu England limefungwa rasmi jana Mei 28, 2023 huku Leicester City na Leeds United zikiungana na Southampton kushuka daraja kwenda Ligi ya Championship
Klabu ya Everton imenusurika kushuka daraja kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Bournemouth huku Chelsea ikimaliza ikiwa nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi
Bingwa ni Manchester City huku Arsenal, Man United na Newcastle United zikimaliza katika nafasi ya pili, tatu na nne
Liverpool na Brighton zitacheza Europa League msimu ujao huku Aston Villa ikiambulia nafasi ya kucheza UEFA Conference League
Erling Haaland ameshinda tuzo mchezaji bora wa Ligi Kuu ya 2022/2023 huku pia akishinda tuzo ya PFA



