Rasmi Mauricio Pochettino amesaini mkataba wa kuifundisha Chelsea, makubaliano baina ya pande hizo mbili yalifanyika wiki mbili zilizopita
Mwandishi maarufu wa habari za michezo zenye uhakika Fabrizio Romano alithibitisha jana
Taarifa ya Romano imeeleza kuwa Chelsea watamtangaza Pochettino muda wowote kuanzia sasa kuwa kocha mpya kwa mkataba wa miaka mitatu
Kocha huyo wa zamani wa Spurs ataanza kazi wiki ijayo baada ya jana kuhitimishwa msimu wa Ligi Kuu England
Lampard ameondoka rasmi baada ya msimu kumalizika huku Chelsea ikimaliza katika nafasi ya 12