Simba yampeleka Manula kutibiwa Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th May 2023


Simba yampeleka Manula kutibiwa Afrika Kusini

Mlinda mlango namba moja wa Simba Aishi Manula ameondoka nchini jana kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ya nyama za paja

Manula alipata majeraha katika mchezo wa Robo Fainali ya Azam Sports Federation Cup dhidi ya Ihefu FC uliopigwa Uwanja wa Azam Complex, Aprili 7

Daktari wa Simba, Edwin Kagabo ambaye ameongozana na Manula amesema mlinda mlango huyo atafanyiwa upasuaji ikiwa ni sehemu ya matibabu yake

Kagabo amesema watafikia katika Jiji la Johannesburg na ndipo upasuaji na matibabu yake yatafanyika

"Tunaondoka kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ya mlinda mlango wetu Aishi. Matibabu yake yatahusisha upasuaji kwahiyo kuhusu atakuwa nje kwa muda gani itategemea na upasuaji huo," amesema Dk. Kagabo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.