Mlinda mlango namba moja wa Simba Aishi Manula ameondoka nchini jana kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ya nyama za paja
Manula alipata majeraha katika mchezo wa Robo Fainali ya Azam Sports Federation Cup dhidi ya Ihefu FC uliopigwa Uwanja wa Azam Complex, Aprili 7
Daktari wa Simba, Edwin Kagabo ambaye ameongozana na Manula amesema mlinda mlango huyo atafanyiwa upasuaji ikiwa ni sehemu ya matibabu yake
Kagabo amesema watafikia katika Jiji la Johannesburg na ndipo upasuaji na matibabu yake yatafanyika
"Tunaondoka kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ya mlinda mlango wetu Aishi. Matibabu yake yatahusisha upasuaji kwahiyo kuhusu atakuwa nje kwa muda gani itategemea na upasuaji huo," amesema Dk. Kagabo



