Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumanne May 30 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 May 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumanne May 30 2023

Tottenham wamedhamiria kuzima majaribio ya Manchester United ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa England Harry Kane, 29, msimu huu wa joto, huku mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy akigoma kumuuza Kane kwa timu pinzani ya Ligi kuu England. (Mirror)

Erik ten Hag ana imani kuwa anaweza kumshawishi kiungo wa kati wa Chelsea Mason Mount mwenye umri wa miaka 24 ajiunge na Manchester United kama sehemu ya maboresho ya kikosi chake kwenye usajili wa majira ya joto. (Telegraph)

Bayern Munich wako tayari kulipa pauni milioni 95 kumnunua kiungo wa kati wa West Ham na England Declan Rice, huku timu hiyo ya Ujerumani ikiwa na nia ya kuipiku Arsenal katika kuinasa saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Mirror)

Paris St-Germain wana nia ya kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Arsenal na Norway Martin Odegaard mwenye umri wa miaka 24. (Mail)

Tottenham, Newcastle na Arsenal ni miongoni mwa vilabu vya Ligi kuu ya England vinavyomtaka James Maddison wa Leicester. Kiungo huyo wa kati wa England mwenye umri wa miaka 26 anaweza kununuliwa kwa takriban £40m. (Mirror)

Crystal Palace wamemtafuta mkufunzi wa zamani wa Chelsea na Brighton Graham Potter kuziba nafasi ya kocha iliyo wazi, huku Nice pia ikimtaka Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 48. (Footmercato)

Liverpool wamekataa ofa ya kudumu ya uhamisho kutoka nje ya nchi kwa kiungo mshambuliaji wa Ureno chini ya umri wa miaka 21 Fabio Carvalho huku klabu hiyo ya Merseyside ikifikiria kumtoa kwa mkopo tu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (Athletic)

West Ham wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumnunua James Ward-Prowse, huku Southampton wakisema thamani ya kiungo huyo wa kati wa England mwenye umri wa miaka 28 ni pauni milioni 40. (Sun)

Newcastle wana imani kuwa kiungo wa kati wa Brazil Bruno Guimaraes, 25, atasaini kandarasi mpya huko St James' Park licha ya kutakiwa na Barcelona. (90Min)

Mshambulizi wa Brazil Roberto Firmino, 31, ambaye ataondoka Liverpool msimu huu wa joto, anasubiri kuona kama atafaa kwenye mipango ya Real Madrid kabla ya kuchukua uamuzi wa kuhamia Hispania. (Mail)

Kocha wa Barcelona Xavi amekiri kuwa yuko kwenye mazungumzo na mshambuliaji wa Argentina na Paris St-Germain Lionel Messi mwenye umri wa miaka 35 kuhusu kurejea Camp Nou msimu wa joto. (Standard)

Everton inamtaka mshambuliaji wa Mali El Bilal Toure mwenye umri wa miaka 21 baada ya kurejea kwenye kikosi cha kwanza cha Almeria siku ya Jumapili. (Mail)

Chelsea wameanzisha mazungumzo kuhusu mpango wa kumsajili kiungo wa kati wa Uruguay na Sporting CP Manuel Ugarte, 22. (90Min)

Crystal Palace wanafikiria kumchukua kwa mkopo kiungo wa kati wa Chelsea na England wa chini ya umri wa miaka 19 Lewis Hall, 18. (Mail)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’