Mlinda lango wa Simba Aishi Manula amekamilisha matibabu Afrika Kusini akitarajiwa kurejea nchini baada ya afya yake kuimarika
Manula alifanyiwa upasuaji siku ya Jumanne katika Hospitali moja katika jiji la Johanesburg
Daktari wa Simba Edwin Kagabo ambaye aliongozana na Manula huko Afrika Kusini, amesema upasuaji ulikwenda salama na siku ya Ijumaa wataruhusiwa kutoka Hospitalini
Hata hivyo Kagabo amesema bado hawajafahamu Manula atakuwa nje kwa muda gani kutokana na aina ya matibabu aliyofanyiwa
Manula alichanika nyama za paja katika mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Ihefu Fc uliopigwa April 7



